Wednesday, January 30, 2013
Wednesday, January 16, 2013
FAIDA ZA KARATE
Faida za karate
•KUPIGANIA MWENENDO SAHIHI WA TABIA
Lengo kuu la karate si ushindi dhidi ya mpinzani au jambo fulani bali ni ushindi
dhidi ya nafsi yako mwenyewe. Hii ndio karate-do. Neno ‘do’ lina maana ya ‘njia’.
Sote tunajua kwamba hakuna mtu kati yetu aliye mkamilifu hivyo basi ni vema
kila mmoja wetu akajitahidi kupunguza madhaifu yake katika safari ya maisha
yake. Hii ndio njia ya karate yaani ‘ karate-do’.
Madhaifu yanayoelezwa hapa ni kama hasira kali, uzinzi, ulevi, aibu iliyokithiri
au kutokujiamini, woga, uvivu, tamaa, husuda, chuki, kujisikia, dharau, majungu n.k.
Ni vema ikaeleweka kwamba sanaa haimjengi mtu bali mtu ndiye
huijenga sanaa ikiwa na maana ya kuifanya karate kuwa sanaa bora na muhimu
katika maisha yetu tofauti kabisa na ambavyo imekuwa ikichukuliwa.
Lakini kamwe karate haitoweza kumsaidia mtu kitabia mpaka pale atakapo pata
mafunzo kutoka kwa mwalimu ambaye ni msomi na mtaalamu wa sanaa hiyo.
Wataalamu na wasomi wa karate wapo wachache mno na walimu wengi si wataalamu
hivyo ni vema kuwa makini mara mtu atafutapo shule ya kujifunza kwasababu ni
vigumu mno kupima utaalamu na elimu ya mwalimu.
•UWEZO WA KUJIHAMI PASIPO KUHITAJI SILAHA
Kama ndege, wanyama na mimea mbalimbali ina namna au mbinu za kujihami
kwanini asiwe binadamu ?!.
Karate inamuwezesha karateka kuweza kujihami katika mazingira hatarishi
pasipo kujali umri, jinsia,nguvu au umbo alilonalo. Itagharimu nguvu ndogo sana
pamoja na ustadi sahihi wa mbinu ya karate katika kuimudu hali ya hatari.
•NIDHAMU NA KUJITAMBUA KATIKA MAZINGIRA MBALIMBALI
Karateka ni lazima muda wote awe mwenye nidhamu, aitambue nafsi yake
pamoja na mazingira yanayomzunguka. Hii itamuwezesha kutimiza wajibu wake pale
atakapo hitajika kufanya hivyo. Lakini pia karateka kama mtu yoyote atakuwa
na marafiki wenye tabia mbalimbali hivyo kuna wakati atatakiwa kuheshimu
maamuzi na mitazamo yao pindi watakapo kuwa pamoja. Hii kwenye karate
tunaita ‘ roho yenye muafaka ‘.
•AFYA NJEMA ILIYO IMARA
Karate inamsaidia karateka katika kuimarisha afya yake kupitia mazoezi na taratibu
mbalimbali zilizopo mafunzoni. Waweza kuitumia karate katika kupunguza uzito
wa mwili, kujenga misuli yenye nguvu, kujenga mifupa na viungo imara n.k.
•MTU YEYOTE ANAWEZA KUJIFUNZA KARATE
Tofauti na sanaa nyingi za mapigano, karate haimbagui mtu katika mafunzo yake.
Pasipo kujali jinsia, umri, nguvu au umbo; mtu yeyote anaweza kuanza mafunzo
ya karate hata kama ana umri wa miaka hamsini(50) na kuendelea alimradi
atakuwa akifundishwa na mwalimu mtaalamu na msomi wa karate ambaye ataweza
kutofautisha mafunzo kulingana na umri, jinsia, nguvu na umbo la mwanafunzi.
Monday, January 14, 2013
Subscribe to:
Posts (Atom)